Nafasi Ya Matangazo

July 16, 2016

Augustine Lyatonga Mrema-Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole
*****
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa mamlaka aliyopewa amefanya uteuzi wa viongozi na watendaji wa taasisi mbalimbali za Serikali, na pia amewapandisha vyeo maafisa wa Jeshi la Polisi Tanzania.

Uteuzi huo ni kama ifuatavyo;

Mhe. Augustino Lyatonga Mrema.
Ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole kwa kipindi cha miaka mitatu, kuanzia leo tarehe 16 Julai, 2016.

Mhe. Augustino Lyatonga Mrema anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Jaji Mstaafu Mhe. Eusebia Nicholaus Munuo ambaye muda wake umemalizika.

Prof. William R. Mahalu
Ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete. Uteuzi huu umeanza leo tarehe 16 Julai, 2016.

Prof. Mohamed Janabi
Ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete. Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.

Prof. Angelo Mtitu Mapunda
Ameteuliwa kuwa Kamishna wa Tume ya Utumishi wa Mahakama kwa kipindi cha miaka mitatu. Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.

Bi. Sengiro Mulebya
Ameteuliwa kuwa Kamishna wa Tume ya Utumishi wa Mahakama kwa kipindi cha miaka mitatu. Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.

Bw. Oliva Joseph Mhaiki
Ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC). Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.

Mwl. Winifrida Gaspar Rutaindurwa
Ameteuliwa kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC). Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.

Dkt. Charles Rukiko Majinge
Ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini ya Hospitali ya Taifa Muhimbili. Uteuzi huu umeanza leo tarehe 16 Julai, 2016.

Dkt. Julius David Mwaiselage
Ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taasisi ya Saratani ya Ocean Road. Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.

Kupandishwa Vyeo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewapandisha vyeo maafisa 25 wa Jeshi la Polisi kutoka cheo cha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) na kuwa Naibu Kamishna wa Polisi (DCP).

Waliopandishwa vyeo hivyo ni kama ifuatavyo;

Essaka Ndege Mugasa
Adamson Afwilile Mponi
Charles Ndalahwa Julius Kenyela
Richard Malika Revocatus
Geofrey Yesaya Kamwela
Lucas John Mkondya
John Mondoka Gudaba
Matanga Renatus Mbushi
Frasser Rweyemamu Kashai
 Ferdinand Elias Mtui
 Germanus Yotham Muhume
 Fulgence Clemence Ngonyani
 Modestus Gasper Lyimo
 Mboje John Shadrack Kanga
 Gabriel G.A. Njau
 Ahmed Zahor Msangi
 Anthony Jonas Rutashubulugukwa
 Dhahir Athuman Kidavashari
 Ndalo Nicholus Shihango
 Shaaban Mrai Hiki
 Simon Thomas Chillery
 Leonard Lwabuzara Paul
 Ahmada Abdalla Khamis
 Aziz Juma Mohamed
 Juma Yussuf Ally

Aidha, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewapandisha vyeo maafisa wa Jeshi la Polisi wengine 34 kutoka cheo cha Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) na kuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP).

Waliopandishwa vyeo hivyo ni kama ifuatavyo;

Fortunatus Media Musilimu
Goyayi Mabula Goyayi
Gabriel Joseph Mukungu
Ally Omary Ally
Edward Selestine Bukombe
Sifael Anase Mkonyi
Naftari J. Mantamba
Onesmo Manase Lyanga
Paul Tresphory Kasabago
 Dadid Mshahara Hiza
 Robert Mayala
 Lazaro Benedict Mambosasa
 Camilius M. Wambura
 Mihayo Kagoro Msikhela
 Ramadhani Athumani Mungi
 Henry Mwaibambe Sikoki
 Renata Michael Mzinga
 Suzan Salome Kaganda
 Neema M. Mwanga
 Mponjoli Lotson
 Benedict Michael Wakulyamba
 Wilbroad William Mtafungwa
 Gemini Sebastian Mushi
 Peter Charles Kakamba
 Ramadhan Ng'anzi Hassan
 Christopher Cyprian Fuime
 Charles Philip Ulaya
 Gilles Bilabaye Muroto
 Mwamini Marco Lwantale
 Allute Yusufu Makita
 Kheriyangu Mgeni Khamis
 Nassor Ali Mohammed 
 Salehe Mohamed Salehe
 Mohamed Sheikhan Mohamed
Maafisa hawa wa Jeshi la Polisi Tanzania wamepandishwa vyeo kuanzia tarehe 15 Julai, 2016.


Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
16 Julai, 2016
Posted by MROKI On Saturday, July 16, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo