Nafasi Ya Matangazo

April 16, 2015

Meneja Ufundi Idara ya Petroli EWURA Ndugu Gerald Maganga akiwasilisha moja ya mada katika Semina kwa Wafanyabiashara wa Mafuta Mikoa ya Rukwa na Katavi katika ukumbi wa Moravian Centre Mjini Sumbawanga tarehe 15 April 2015. Kushoto ni Afisa Uhusiano EWURA Ndugu Wilfred Edwin. Miongoni mwa mada zilizowasilishwa katika Semina hiyo ni Udhibiti na Kanuni za Ukokotoaji wa bei za Mafuta, Ubora wa Miundimbinu, Usalama na Utunzaji wa Mazingira katika Sekta ya Mafuta ya Petroli, Faida za kutumia Mafuta yenye kiwango kidogo cha Sulphur na Sheria na Kanuni katika udhibiti wa Sekta ya Petroli nchini.
Afisa Biashara Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Ndugu Paul Nganyanyuka akichangia moja ya mada katika Semina hiyo ya EWURA na wafanyabiashara ya mafuta Mikoa ya Rukwa na Katavi iliyofanyika katika Ukumbi wa Moravian Centre mjini Sumbawanga tarehe 15/04/2015.
 Sehemu ya wajumbe katika Semina hiyo ambao ni wafanyabishara wa vituo vya mafuta Rukwa na Katavi, Mtoa huduma Serikalini GPSA na Maafisa Biashara kutoka Mikoa ya Rukwa na Katavi.
(Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa @Rukwareview.blogspot.com)
Posted by MROKI On Thursday, April 16, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo