Nafasi Ya Matangazo

April 23, 2014

Na Josephat Lukaza wa Proin Promotions Limited - Mbeya
Shindano la Tanzania Movie Talents Kwa kanda ya Nyanda ya Juu Kusini, Mkoani Mbeya limefikia Tamati hapo jana kwa washindi watatu kutoka kanda hii ya nyanda ya juu Kusini Kupatikana na Kutangazwa na Majaji watatu.
Washindi waliotangazwa na Jaji Mkuu wa Shindano hilo, Roy Sarungi kwa kushirikiana na Majaji wawili Single Mtambalike na Yvonne Chery ni Steven Mapunda, Issalito Issaya na Mtawa Kaparata "BABU"
 
Mmoja kati ya washindi watatu waliopatikana Jana na Kutangazwa na Jaji Mkuu wa Shindano hilo Roy Sarungi ni mchezaji wa zamani wa timu ya mpira wa Miguu ya Majimaji ya Songea, Bw Mtawa Kaparata.

Mtawa Kaparata aliibuka mshindi kwa kuweza kuonyesha kipaji chake cha kuigiza achilia mbali uwezo wa mpira aliokuwa nao kipindi hiko.

Kwa upande wake mmoja wa washindi wa Shindano la Tanzania Movie Talents ambae pia alikuwa mchezaji wa zamani wa Majimaji ya Songea , Bwa Mtawa Kaparata alithibitisha kuwa 'Tanzania Movie Talents imepokelewa vizuri na watanzania wa Mkoa wa Mbeya  kwani  ameona usaili ulivyokuwa mgumu kutokana na vipaji vilivyoonyeshwa na vijana wengi waliojitokeza na kuona ongezeko la washiriki waliojitokeza kwaajili ya usaili wa kushiriki katika Shindano hili kubwa na la kwanza Afrika Mashariki na Kati. 

Hii nikutokana na ukweli kwamba washiriki wote wanaofika kwaajili ya Usaili hawatozwi kiasi chochote cha pesa kutoka timu ya Tanzania Movie Talents na pia kufurahishwa na uamuzi wa Majaji wa Timu ya Tanzania Movie Talents,  niwazi kabisa kuwa kutotozwa kwa kiasi chochote cha pesa kwa washiriki kumekuwa ni kivutio kikubwa kabisa hivyo kuongeza idadi ya washiriki katika kila Kanda tunayoenda"alisema Mtawa Kaparata Mkazi wa Mkoa wa Mbeya, Eneo la Soko Matola.

Shindano hili kwa kanda ya nyanda Ya juu kusini limehitimishwa rasmi jana kwa washindi watatu kupatikana na hatimaye shindano hili litahamia Kanda ya Kusini na Usaili utafanyika Mkoani Mtwara 

Shindano hili limelenga kuinua na kukuza vipaji vya kuigiza Tanzania na hatimaye kuendeleza vipaji hivi vya kuigiza Tanzania.
Usaili wa Shindano hili ni bure kabisa na fomu hupatikana eneo la usaili.
Posted by MROKI On Wednesday, April 23, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo