MAANDALIZI ya Redds Miss Moshi 2013 yatakayofanyika Jumamosi, May 18 katika ukumbi wa Aventure, Mjini hapa yameanza kushika kasi.
Akizungumza na Tanzania Daima, mratibu wa mashindano hayo, Mkurugenzi
wa kampuni ya New Vision plan inayohusika na kazi za kuandaa mashindano ya ulimbwende, Moses Komba alisema kuwa jumla ya walibwende wapatao kumi19 watachuana kumsaka malkia wa Moshi.
Moses alisema tayari mchujo wa kwanza umeshafanyika ambapo warembo wote wameshaingia kambini kujifua na kuongeza kwamba mashindano ya mwaka ambayo ni ya pili tangu yaanzishwe yatakuwa ni ya aina yake.





















