Nafasi Ya Matangazo

May 17, 2013

MAANDALIZI YA REDDS MISS MOSHI YASHIKA KASI.

MAANDALIZI ya Redds Miss Moshi 2013 yatakayofanyika Jumamosi, May 18 katika ukumbi wa Aventure, Mjini hapa yameanza kushika kasi.

Akizungumza na Tanzania Daima, mratibu wa mashindano hayo, Mkurugenzi wa kampuni ya New Vision plan inayohusika na kazi za kuandaa mashindano ya ulimbwende, Moses Komba alisema kuwa jumla ya walibwende wapatao kumi19 watachuana kumsaka malkia wa Moshi.

Moses alisema tayari mchujo wa kwanza umeshafanyika ambapo warembo wote wameshaingia kambini kujifua na kuongeza kwamba mashindano ya mwaka ambayo ni ya pili tangu yaanzishwe yatakuwa ni ya aina yake.

Kinywaji cha Chilly Willy yamwag vifaa kwa Taswa FC, Taswa queens

Meneja Masoko wa kinywaji cha Chilly Willy kinacho sambazwa na kampuni ya TSN Group, Yohana Manoli  (Kushoto) akimkabidhi jezi mwenyekiti wa Taswa FC, Majuto Omary (wa kwanza kulia) katika hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika kwenye mgahawa wa Hadees. Kulia ni Meneja Uhusiano wa TSN Group, Meshack Nzowah.

DRAFT 3-The Natural Gas Policy of Tanzania-2013

Draft 3- The Natural Gas Policy of Tanzania -2013to be presented to MPs tomorrow
Kesho jumamosi wabunge tumealikwa kwenye semina kuhusu sera ya Gesi Asilia. Tumegawiwa tayari nakala zetu, tena zipo kwenye lugha ya kimombo.
Ikumbukwe kwamba kuanzia tarehe 22 - 23 Mei 2013 kutakuwa na mjadala wa bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini. Semina hii ni maandalizi ya Bajeti hii.
Jambo la kushangaza ni kwamba wakati sera ya Gesi Asilia ipo kwenye rasimu na ndio kwanza wabunge tumeletewa kutoa maoni, Serikali tayari imetangaza tena kugawa vitalu vya Mafuta na Gesi kwenye Bahari kuu na Ziwa Tanganyika Kaskazini.

MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII PAMOJA NA SSRA YATOA MISAADA KATIKA WODI YA WAZAZI YA CHIKANDE PAMOJA NA KITUO CHA WATOTO WENYE ULEMAVU WA AKILI CHA MIYUJI


Mkuu wa Kitengo cha uhusiano bi Sara Msika akikabidhi msaada wa shuka 100 na magodoro 30 katika wodi ya wazazi ya chikande

Mkuu wa kitengo cha uhusiano cha SSRA Bi Sara Msika akiwa amembeba mmoja kati ya watoto waliozaliwa katika Hospital ya Genera,  wodi ya wazazi ya Chikande mkoani Dodoma..

Wawakilishi wa Mifuko ya hifadhi ya jamii pamoja na SSRA wakikabidhi msaada wa vifaa vya ujenzi katika kituo cha kulea watoto wenye ulemavu wa akili cha Miyuji Cheshire mkoani Dodoma.

PRADO INAUZWA

PRADO TX IN GOOD CONDITION
Model: 1997
Millage: 115,000km
Cc  3000
Engine 1KZ Diesel,
Color: Green 2 tone
Transmission:  AT
5doors, 8passengers, AC, PS, PW, AL, ABS.
Price: Tsh 19m/- Negotiable
TEL: 0712155221/0784587088
E-MAIL:badijohn30@yahoo.co.uk

May 15, 2013

BODA TU BODA YA MWANA MAMA WA MTWARA

 Pikipiki ilirukiwa fasta na Mwana mama huyu, wasio mfahamu wengi walimshangaa, alivaa Kofia ngumu kisha akapachika pochi yake anapotaka na kisha akaiwasha. Huu ni usafiri wake anaoumiliki na huutumia mara zote katika mishe mishe zake.
 Safari ikaanza na gia ziilingizwa... mama huyu ni maarufu sana Mjini Mtwara
Truuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu........nilikuwa naona vumbi tu linatimka na masihara niliyodhani anafanya kumbe ndio alikuwa akiondoka na huo ndio usafiri wake.

SSRA NA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII YATOA ELIMU KWA WABUNGE PAMOJA NA WAANAHABARI KATIKA MAONESHO YA WIKI YA HIFADHI YA JAMII MJINI DODOMA

 Mkurugenzi Mkuu wa SSRA Bi Irene Isaka akiwasilisha mada kuhusu sekta ya hifadhi ya jamii kwa waheshimiwa wabungePicha 6: Mkurugenzi Mkuu wa GEPF Bw Daud Msangi akiwasilisha mada juu ya mchango wa GEPF katika kuendeleza sekta ya hifadhi ya jamii
 Waziri wa Kazi na Ajira Mhe. Gaudentia Kabaka akifungua rasmi semina ya waandishi wa habari iliyoandaliwa na SSRA na Mifuko ya Hifadhi ya jamii 
  Mkurugenzi Mkuu wa SSRA BI Irene Isaka akijibu baadhi ya maswali ya waandishi wa habari. Pembeni yake ni waziri wa kazi na ajira Bi Gaudentia Kabaka pamoja na naibu waziri Dr Milton Makongoro Mahanga

CCM MOSHI WAGOMEA DARAJA LA RAU MBOKOMU

Sehemu la Daraja la Rau, lililoko katika manispaa ya Moshi, Mkoani Kiliamnajro lililokataliwa na Viopngozi wa CCM wilaya ya Moshi katika ziara ya kukagua miradi ya manispaa Moshi ili kujiridhisha kama miradi inayoendeshwa na Manispaa hiyo ianendena na kiwango kinachotakiwa.

 Wajumbe wakijadiliana jambo wakati wakikagua miradi mbalimbali ya maeneleo.

Katibu wa CCM, Aluu Segamaba akiongoza viongozi wenzake kukagua daraja la Rau linadaiwa kujengwa kwa kutumia kiasi cha sh. milioni 102, lililokatika kabla ya ujenzi wake kukamilika, viongozi wamelikataa daraja hilo.  

KITABU CHA MWAKALEBELA HADHARANI MECHI YA WATANI WA JADI

Na Mwandishi Wetu
KITABU cha kwanza nchini kinachozungumzia soka la Tanzania kijulikanacho kwa jina la “Soka la Tanzania” kitaanza kuuzwa siku ya mechi ya watani wa Jadi, Yanga na Simba iliyopangwa kufanyika Jumamosi kwenye uwanja wa Taifa.
 
Akizungumza na jijini jana, mtunzi wa kitabu hicho, Katibu Mkuu wa zamani wa Shirikisho la Kandanda nchini (TFF), Fredrick Mwakalebela alisema kuwa maandalizi ya zoezi hilo yamekamilika na yamedhaminiwa  na kampuni TSN Group kupitia kinywaji chake cha kuongeza nguvu Chilly Willy, Events World, Vannedrick Tanzania Limited na  Inbox Pub.
 
Wadhamini wengine ni Clouds FM, Times FM na Street Soul kwa mujibu wa Mwakalebela. Alisema kuwa kwa sasa ametoa nakala 10,000 kwa ajili ya kuuzwa Tanzania nzima. Alisema kuwa kitabu hicho kimezungumzia historia ya soka la Tanzania katika Nyanja za vijana, wanawake na wanaume, ligi kuu ya Tanzania Bara, Taifa Cup, Timu ya Taifa na Utawala Bora.

WAHI TIKETI YAKO YA KUCHANGIA AFYA YA UZAZI WA MAMA NA MTOTO


WANYWAJI WAPINGA VIROBA KUPIGWA MARUFUKU

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda na Biashara, wakiangalia uzalishaji walipotembelea kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), Dar es Salaam hivi karibuni.
 ************

Na Mwandishi Wetu.
BAADHI ya wananchi jijini Dar es Salaam, wamelalamikia hoja iliyozuka bungeni wiki hii kwamba kinywaji cha Konyagi aina ya Kiroba kipigwe marufuku nchini.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi hao, walisema endapo serikali itachukua uamuzi wa kupiga marufuku kinywaji hicho, watarudia kunywa pombe aina ya gongo ambayo ni hatari kwa afya zao.

Mkazi wa Mbagala, Faustine Mwiruka aliyekutwa kwenye baa ya Kisuma, aliiasa Serikali kutothubutu kukubali kinywaji hicho kupigwa marufuku, kwani ikifanya hivyo wengi wa wananchi wenye kipato cha chini wataanza tena kunywa gongo na pombe za kienyeji.

MICROSOFT, UHURU ONE WAANZA MAJARIBIO YA TEHAMA

 Mkurugenzi wa Masuala ya Sheria na Uhusiano wa Microsoft Africa, Louis Otieno,  Louis Onyango Otieno akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mihayo Wilmore na Mkurugenzi wa Utambuzi COSTECH, Faith Shimba.
DAR ES SALAAM, Tanzania
KAMPUNI za Microsoft na Uhuru One, wameanza mpango wa majaribio wa utoaji wa elimu ya Teknolojia ya Mawasiliano (Tehama) kwa kutumia mkongo wa Taifa kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu lengo likiwa kuibua uvumbuzi mpya katika sekta hiyo.

Akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Masuala ya Sheria na Uhusiano wa Microsoft Africa, Louis Otieno alisema mpango huo utachukua miezi sita hadi mwaka mmoja.

May 14, 2013

PENDEKEZO BINAFSI LA MBUNGE ZITTO KABWEKUHUSU KUZUIA UNYONYAJI DHIDI YA WASANII WA TANZANIA KATIKA BIASHARA YA MIITO (RING BACK TONES)

Kwenda kwa:          DR ABDALLAH KIGODA, Waziri wa Viwanda na Biashara

Kuhusu:                    BIASHARA YA MIITO YA SIMU (RINGBACK TONES)

Kumekuwa na malalamiko makubwa sana kuhusu biashara ya mauzo ya nyimbo kama miito kwenye simu. Malalamiko haya yalianzia kwa wasanii wenyewe na baadaye mimi binafsi niliwasilisha hoja zao Bungeni mwaka 2012. Hata hivyo, hadi sasa malalamiko haya bado hayajapatiwa ufumbuzi na hivyo wasanii kuendelea kunyonywa. Tatizo kubwa katika biashara hii ni USIRI na UNYONYAJI kwa wasanii wa Tanzania.  Suala la USIRI lipo Wizara  ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia.  Suala la Unyonyaji lipo Wizara ya Viwanda na Biashara.

USIRI
Biashara hii ya “Ring Back Tones” (RBT)  hufanywa na Kampuni za simu (Network providers) kwa kununua maudhui kutoka wachuuzi (Content Providers) ambao  nao huingia mikataba na Wasanii (Content Creators).

MAOFISA WA JESHI KUTOKA CHUO CHA KIJESHI GHANA WATEMBELEA TBL DAR

 Meneja Uhusiano wa TBL, Doris Malulu (kulia) akitoa maelezo kwa maofisa hao kuhusu shughuli mbalimbali za kampuni hiyo.
Maofisa wa Jeshi kutoka Chuo cha Ukamanda na Unadhimu cha Ghana, wakitembelea Kiwanda cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Dar es Salaam, kwa lengo la kujenga ushirikiano katika nyanja za Sayansi, Teknolojia, Kiuchumi na Kijamii.Maofisa wanaosoma katika chuo hicho wanatoka Afrika Kusini, Nigeria, Ivory Coast, Togo, Rwanda na Ghana.

TUJIAMINI KIKUNDI CHA USINDIKAJI KOROSHO CHA AKINA MAMA WA LINDI

 
 Katibu wa Kikundi cha Usindikaji Korosho cha Tujiamini akipanga pakiti za Korosho tayari kwa kuwauzia wateja katika Stand kuu ya Mabasi Lindi Mjini.
Mkoa wa Llindi wakazi wake wengi ni wakulima hasa maeneo ya vijijini wengi wanalima mazao mchanganyiko yaani ya biashara na chakula mazao ya biashara hasa ni Korosho ambazo zinapatika kwa wingi katika wilaya ya Ruangwa,Lindi Vijijini,na Nachingwea.

Pia kuna zao la Ufuta na ndizi kama zao la biashara na chakula pia Mazao ya chakula kuna mahindi,mpunga,muhogo,nyanya,vitunguu hizi pia ulimwa sana wakati wa masika kutegemea na mvua za vuli.

Biashara wakazi wengi wa mkoa wa Lindi wanafanya biashara hasa biashara ndogondogo zijulikanaza kama machinga trade wanauza mazao wakati wa mavuno na uchukua bidhaa nyingi kutoka Dar-es-Salaam na kupeleka vijijini hasa kwenye Kata.

LINDI MKOA UNAOHITAJI JICHO LA ZIADA KATIKA MIUNDOMBINU

 Mnara maalum ambao unautambulisha mkoa wa Lindi.
Camera ya Father Kidevu Blog leo imevinjari na kupata taswira kadhaa za mji wa Lindi.

Licha ya Mkoia huu kuanzishwa tangu mwaka 1971 ukiwa na ukubwa wa eneo Kilometa za mraba 67,000 km². Karibu robo ya eneo lake au 18,000 km² ni sehemu ya hifadhi ya wanyama ya Selous.

Mkoa wa Lindi umepakana na mikoa ya Pwani, Mtwara, Ruvuma na Morogoro. Upande wa mashariki hupakana na Bahari Hindi.

Mkoa una wilaya sita za Lindi Mjini, Lindi Vijijini, Kilwa, Nachingwea, Liwale na Ruangwa.

REDD'S MISS UBUNGO 2013 KUPATIKANA IJUMAA MEI 17

Baadhi ya washiriki wa Shindano la Redd's Miss Ubungo 2013 wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa mazoezi yao  jana. Warembo hao wanataraji kupanda jukwaani Ijumaa ya Mei 17, mwaka huu katika Ukumbi wa Meeda uliopo Sinza jijini Dar es Salaam na kusindikizwa na kundi zima la FM Academia wazee wa Ngwasuma.

MEYA WA ILALA AFUNGUA TAWI JIPYA LA DStv KARIAKO JIJI DAR

Muonekano wa nje wa Ofisi za DStv Tanzania zilizopo barabara ya Msimbazi - Kariakoo karibu kabisa na Diamond Trust Bank jijini Dar es Salaam.
Meneja Uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo na Meneja Masoko wa Kampuni hiyo Furaha Samalu katika hatua za mwisho za maandalizi kabla ya kuwasili kwa mgeni rasmi.
Meneja Mkuu wa Multichoice Tanzania Bw. Peter Fauel akisalimiana na Mgeni rasmi Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa mara baada ya kuwasili kuzindua tawi jipya la ofisi za DStv Tanzania lilolopo Kariakoo barabara ya Msimbazi karibu na Diamond Trust Bank jijini Dar. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Multichoice Tanzania Balozi Ami Mpungwe.

CRDB YAFANYA MKUTANO MKUU WA 18 WA WANAHISA JIJINI ARUSHA

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei, akitoa mada wakati wa Mkutano Mkuu wa 18 wa Wanahisa wa benki hiyo uliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa AICC jijini Arusha, mwishoni mwa wiki. 
Mmoja wa wajumbe wa mkutano Mkuu wa 18 wa Wanahisa wa CRDB akiwa katika maandalizia ya kuingia katika ukumbi wa  mikutano wa AICC jijini Arusha.
 Mtangazaji Mkongwe, SalimMbonde (kulia) akifuatilia Mkutano Mkuu wa  18 wa Wanahisa wa CRDB uliofanyika jijini Arusha mwishoni mwa wiki.

May 13, 2013

12 KUWANIA TAJI LA MISS LINDI 2013 MEI 31.

Shindano la kumsaka Malkia wa Mkoa wa Lindi ‘Miss Lindi 2013’ linataraji kufanyia Mei 31 mwaka huu katika ukumbi wa Hoteli ya Lindi Beach Resort (Oceanic Hotel).

Akizungumza na Father Kidevu Blog mjini Lindi, Mwandaaji wa Shindano hilo, Shaha Ramadhani kupitia kampuni ya Alliance Entertainment amesema warembo 12 wataingia Kambini Hotelini hapo chini ya Mkufunzi Zainab Mselem ambaye alikuwa Miss Pwani 2010.

Maandalizi yote ya shindano hilo yanaendelea vyema na Milango io wazi kwa Wadhamini kujitokeza.

Maandalizi yote ya shindano hilo yanaendelea vyema na Milango io wazi kwa Wadhamini kujitokeza. 

Irine Veda (pichani juu) ndiye anashikilia taji hilo baada ya kulitwaa mwaka 2012. 

SOMANGA NA UUZAJI SAMAKI

 Mkazi wa Kijiji cha Somanga Wilayani Kilwa, Kando ya Barabara kuu ya Lindi Rufiji Mkoani Pwani akiuza samaki kwa abiria na wasafiri mbalimbali watumiao barabara hiyo. Biashara ya Samaki hufanywa zaidi na akina mama na wasichana wadogo kwa lengo la kujipatia kipato na kuweza kuyaendesha maisha yao ya kila siku.
 Hawa ndio Samaki wenyewe.
Wateja mbalimbali wakila Samaki eneo la Somanga...

ST.JONH MABINGWA SAFARI LAGER HIGHER LEARNING POOL COMPETITION 2013.

  Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amosi Makalla (mwenye suti) akifurahi pamoja na wachezaji wa chuo cha St.John’s  mara baada ya kutwaa ubingwa wa ‘Safari Lager Higher Learing Pool Competition 2013’  Mkoa wa Dododma.
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amosi Makalla (katikati) akimkabidhi nahodha wa chuo kikuu cha St.John’s, Mkole Mpangala  fedha taslim Sh.500,000 mara baada ya kutwaa ubingwa wa mashindano ya ‘Safari Lager Higher Learing Pool Competition 2013’  katika mkoa wa Dodoma, (wa pili kushoto), mwenyekiti wa chama cha mchezo huo mkoani Dodoma,Fred Mushi. na Mradsibu wa Mashindano,Chavalimembe Lutambi.

MWENYEKITI WA CCM THEMI ARUSHA AHAMIA CUF AKAGOMBEE UDIWANI

https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/?ui=2&ik=415872e567&view=att&th=13e9d71885d26eec&attid=0.1&disp=inline&safe=1&zw&saduie=AG9B_P9g9RL3KZvavfSalyyJf1ib&sadet=1368442269914&sads=yanlPFIzNXWmv-DkXJGw_Przmj4Aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM kata ya Themi Petro Ndarivoi akirudisha kadi ya chama cha Mapinduzi kwa mwenyekiti wa chama cha CUF halmashauri ya jiji la Arusha Hamza Mustaph kwenye makao makuu ya chama hicho jana jioni
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/?ui=2&ik=415872e567&view=att&th=13e9d782d03d8119&attid=0.1&disp=inline&safe=1&zw&saduie=AG9B_P9g9RL3KZvavfSalyyJf1ib&sadet=1368442200954&sads=PTi5ICp4_AzABeyERCl15x563x4 
Mgombea udiwani kwa tiketi ya chama cha wananchi CUF kata ya Themi kwenye uchaguzi utakaoanza wiki ijayo Petro Ndarivoi akizungumza na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya CUF halmashauri ya jiji la Arusha jana jioni wakati aliporudisha rasmi kadi ya ccm na kuchuwa kadi ya CUF mbele ya mgombea udiwani kwenye kata ya ELERAI John Bayo na mwenyekiti wa CUF wilaya ya Arusha Hamza Mustapha. Picha: Mahmoud Ahmad Arusha.

SIKU YA WAUGUZI DUNIANI, MEI 12, ILIVYOFANA MKOANI MOROGORO


 


Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha uuguzi cha Mkoa wa Morogoro ( PHN) wakishikilia mabango yenye ujumbe mbalimbali wakati wa maadhimisho ya siku ya wauguzi duniani , Mei 12, siku hiyo wauguzi wote duniani wanamkumbuka muasisi wa uuguzi,  mama  Florence Nightngale ambaye alizaliwa kwenye familia tajiri nchini Italia , kimkoa yalifanyika  Manispaa ya Morogoro na mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa Mkoa huo, Joel Bendera.

MACHAVA FC YAPOKEA VIFAA NA FEDHA TASLIMU KUTOKA KWA WADAU WA SOKA KILIMANJARO

Mwandishi Wetu, Moshi
KATIKA kuelekea mchezo wa jana dhidi ya Flamingo FC ya Arusha, Machava FC ambo ndio mabingwa wa ligi daraja la Tatu, mkoa wa Kilimanjaro, wamekabidhiwa vifaa vya michezo na uongozi wa chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Moshi.

Machava FC walikabidhiwa vifaa hivyo ambavyo ni mipira mitano na Jezi, kama sehemu ya mchango wa Chama hicho kwa timu hiyo ambayo kwa sasa ndio inayobeba Roho ya mkoa wa Kilimanjaro katika medani ya soka.

Akizungumza baada ya kukabidhi vifa hivyo vilivyotolewa kwa timu hiyo na Mjumbe wa Halmashauri kuu CCM, Jerry Silaa, Katibu wa CCM wilaya ya Moshi Mjini Aluu Segamba aliwahakikishia wapenzi wa soka mkoani hapa kuwa wako tayari kushirikiana nao hadi mwisho wa Safari.

“Leo tunatimiza ahadi yetu kwa wawakilishi wetu, mabingwa wa Mkoa timu ya Machava, tunaamini kuwa timu hii kama roho ya kilimanjaro katika mchezo wa soka itafanya makubwa na kinachotakiwa ni kuwapa sapoti inayostahili,” alisema Segamba.

Share

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More